21 تغريدة 8 قراءة Jul 22, 2023
KWA MTU ANAYEANZISHA UHUSIANO MWA KIMAPENZI.
UZI
Kama utakuwa umefuatilia vizuri utagundua kuwa kuumizwa, kunyanyasika, kupelekeshwa na kuzinguliwa katika mahusiano ni mamlaka ambayo watu huwapa wenzi wao.
Yaani, hakuna namna mtu anaweza kukuzingia, kukuumiza, kukunyanyasa na kukupelekesha atakavyo kama usipompa
mamlaka ya yeye kufanya hivyo.
Yapo mambo mengi ambayo ukiyafanya ya naweza kumpa mwenzi wako nguvu ya
kukupelekesha, kukuumiza na kukubuluza.
Lakini pia yapo mambo ambayo ukiyafanya
hatokuwa na nguvu ya kufanya hivyo.
Prof Bixen. Nimekusogezea hili baada ya kuwa tatizo kwa wengi Dm . Kwa mtu anayeanzisha uhusiano wa kimapenzi, hapa kuna ushauri mzuri:
1. Make Him/Her Know Can Be Replaced.
Yaani mfanye ajue kuwa nafasi yake inaweza ikachukuliwa, pengo lake linaweza likazibwa na historia yake ikasahaulika.
Hii itamfanya ajue kuwa yeye sio BORA kuliko wengine na wala sio kwamba haiwezekani wewe kupata miwngine aliye bora zaidi yake.
Kwa asili, mwanadamu anaanza kujiona na Kuwa msumbufu sana pale atakapogundua kwamba uwepo wake yeye ni wa kipekee.
Wakati wowote mfanye ajue kuwa upo uwezekano wa mtu mwingine kuchukua nafasi aliyopewa yeye.
2. usimfanye akajua kuwa yeye ndio chaguo pekee ulilonalo. Ukimfanya akajua hivyo
atakuwa na jeuri kwamba wewe huna pa kwenda.
kwake umefika, hufurukuti wala
kutingishika, umeshikwa ukashikika, hii inaweza kumfanya akuzingue vibaya sana.
Yawezekana ni kweliyeye ndiye chaguo lako pelee, lakini usijiroge ukamfanya yeye akalijua hilo, atakuumiza na kukutesa sana.
Huku akiamini kuwa HUNA cha KUMFANYA.
3. Jijue mwenyewe:
Elewa thamani yako, malengo yako, na kile unachotaka kutoka kwenye uhusiano kabla ya kuanza.
4. Kuwa wazi:
Wasiliana waziwazi na mpenzi wako kuhusu hisia zako, matarajio, na mahitaji yako
5. Jenga msingi wa urafiki:
Uhusiano mzuri wa kimapenzi unategemea urafiki thabiti. Jitahidi kuwa rafiki na mpenzi wako.
6. Tambua ishara za tahadhari:
Angalia ishara za tahadhari za mpenzi wako, kama vile ukosefu wa heshima, ukosefu wa uaminifu, au udhaifu wa kihisia.
7. Uaminifu:
Kuwa mwaminifu kwa mpenzi wako na uwe waaminifu kwa ahadi zako.
8. Heshima:
Waheshimu mpenzi wako kama mtu binafsi na heshimu mipaka yake na maamuzi yake.
9.Kuwa na uvumilivu:
Uhusiano unahitaji uvumilivu. Tambua kuwa hakuna mtu kamili na kumbuka kuwa kila mtu ana mapungufu yake.
10. Sauti yako:
Usiogope kutoa maoni yako na kuzungumza juu ya mambo muhimu. Hii itasaidia kujenga mawasiliano ya wazi katika uhusiano wako.
11.Kuwa mwepesi kusamehe:
Kusamehe ni muhimu katika uhusiano. Jifunze kusamehe makosa madogo na kusuluhisha mizozo kwa njia yenye heshima.
12. Furahia wakati pamoja:
Weka muda wa kufurahia na kufurahia wakati pamoja. Hii itasaidia kuimarisha uhusiano wako.
13. Kuwa mkarimu:
Jitahidi kuwa mkarimu kwa mpenzi wako, siyo tu kwa vitu vya kimwili, lakini pia kwa upendo, msaada, na kujali.
14. Jifunze kusikiliza:
Uwe tayari kusikiliza mpenzi wako kwa makini na kwa uaminifu. Fikiria hisia na mahitaji yake.
15. Thamini faragha:
Heshimu faragha ya mpenzi wako na usivunje uaminifu kwa kukiuka faragha yake.
16. Kuwa na mipango ya baadaye:
Panga na mpenzi wako juu ya malengo ya baadaye na ndoto zenu. Hii kitu itawafanya kukaa.
Unaweza Bookmarks hii Tweet huenda ukahitaji haya mawazo siku moja au kumsaidia mwenzako.
| Mwisho |
Nashkuru kwa kupitia uzi huu nadhani utakua umejifunza kitu.
Tafadhali nijulishe ikiwa kuna kitu maalum ungependa niandike. Usisahau kulike, Kuretweet , Kufollow @heisbixen na Kucomment.

جاري تحميل الاقتراحات...