Mfalme 👑🇹🇿
Mfalme 👑🇹🇿

@MfalmewaX

35 تغريدة 16 قراءة May 21, 2023
"MWANAMKEEE KAMA WEWE HUKIJUI CHEO CHANGU, ALLAH ANAKIJUA"
UZI🧵~(Dini & Mahusiano)
Huu uzi utakubadilisha sana.
Ndugu zangu siku inakuja haiko mbali
Tatizo letu tuliowengi tumeyasahau majumba yetu, tunaishi na wanawake kienyeji, nje na maagizo ya M/nyezi Mungu.
Allah hataki wewe uishi na mwanamke anataka wewe umuongoze mwanamke.
Hatuongozi tena wanamke ila tunaishi nao, nakwambieni kila anayeishi na mwanamke ajiandae na adhabu kali
Kuishi na Mwanamke ni vipi..!?
Umerudi kwa mke wako, una uliza kuna mtu kanitafuta leo, watoto wameenda shule, kuku uliwafungulia, haya mke wangu nawahi msikitini..
Nikitoka kuswali ntakuja na wageni naomba tuandalie chai,. huko ndo kuishi. Mwanamke
Kuongoza Mwanamke ni vipi..!?
Umerudi, unamuita mkeo serious hakuna mzaha katika Dini, umeswali adhuhuri? Nae atamke nimeswali, Sawa nimekusikia ila hiyo haitoshi magharibi imekaribia...
Nawahi jamaa msikitini, mke wangu maji yale jisafishe uswali usifanye mzaha na swala, Usijiniletea matatizo siku ya kiama.
Ndugu zangu nani leo anafanya hivyo?
Kuongoza mwanamke tenga muda, umeshindwa wiki mara 1 au mwezi mara 1
Siku hiyo ukiingia nyumbani kila kitu zima..
..wape mawaidha au husia,
Mke wangu, wanangu nawakumbusha mauti yanakuja ghafla, hayana taarifa
Mimi ndio baba, siku moja Allah atanichukua bila kutarajia, mke wangu hawa watoto nitakuachia utakuja kuhangaika nao. Wapo wenzako kwenye uso wa dunia wameshafikiwa..
Mke wangu nenda barabarani utaona wenzio wamebeba sinia za matunda na ndizi, wengine wamepanga vitumbua, wengine na watoto mgongoni
Mke yangu haya yanaweza kukufika, Mke wangu wewe ni mjamzito wakati wowote unaweza kujifungua usije ukadhani Allah atakuacha kwa kuwa una kiumbe...
Allah anaweza kuichukua roho yako, wenzako ni wengi wamelala chini wakina na hali kama yako walimezwa na udongo wanaliwa na wadudu na mimba zao
Mke wangu mtii M/nyezi Mungu na mitume. Ndugu zangu na huku ndio kuongoza Mwanamke nani anafanya hivyo?
Sisi leo wake wetu hawaswali
Swalaaa swalaa alfajiri..Bwana anaenda kuswali, Bibi anatoka kuchoma chapati barazani
Maskini mwanamke Kavaa upande wa kitenge, makwapa wazi, Mgongo wazi, Kifua wazi, manywele yametimka kama shetani,
Ana janaba anawachomea watu chapati,
Na huyo bwana akirudi haulizi umeswali, hajali adhabu ya kiama ndio kwanza na yeye mwanaume anasema embu nichome mbili za haraka niwahi
Na akishakula safari, haulizi huko nyuma mmeswali watakutana na Mungu siku ya kiama.
Mwanamke ×3, akimjua Mungu & Dini ikawa ndani yake atakutukuza, atakuthamini, atakupa Hadhi yako,
Utapata utulivu wa nafsi yako, utaheshimika na ukifika nyumbani utahisi mimi ndio mwenye himaya.
Mwanamke kama hakumjua Mungu na ndani ya moyo wake hakuna Dini, atakudharau..
Atakupuuza, utakuwa si lolote si chochote, unaweza kuamrisha jambo na asifanye, na ukamzuia kufanya jambo akafanya, ukamzuia asiende atajibu nitaenda na lolote fanya
Akaoga, akajipamba na kutoka taratibu bila shaka yeyote, utamsindikiza kwa macho
Na utajiuliza ndo unaenda kwel?
Na tulio wengi wake zetu hawana Dini.
Kuna mtu anasoma huu uzi saizj, wallahi akienda kwake kula utamuonea huruma anavyoshambuliwa na mkewe.
Leo mwanamke anaongea na Mume wake ukipita dirishani unaweza kuhisi anaongea na mtoto wa mwisho.
Anafoka, matusi wala hachuji maneno
Jinsi bwana alivyokuwa hana thamani, jinsi anavyoshambuliwa. Haya ndio maisha tunaishi na wanawake.
Thamani ya Mume
Asiyekujua hakuthamini, na kwa kuwa uliyemuoa hana Dini na ndio maana hajui thamani ya mume.
Tuitizame kidogo Thamani ya mume, hata Mwanaume inawezekana hujui
Thamani ya mume, tutatumia Qur'an.
Mwenyezi Mungu subhanallah wa ta'ala anasema.."𝙒𝙖𝙣𝙖𝙢𝙪𝙢𝙚 𝙣𝙙𝙞𝙤 𝙬𝙖𝙨𝙞𝙢𝙖𝙢𝙞𝙯𝙞 𝙬𝙖 𝙬𝙖𝙣𝙖𝙬𝙖𝙠𝙚"
Labda nikuulize , yule anayekusimamia kazini unamuhitaje?
Ni Boss
Vipi Boss wako anapokuita unaingiaje?
kwanza unaangalia shati lako, niko sawa? Yaani hujiamini unakuwa na presha, wakati mwingine utaanza kujiuliza jamani kwa boss hajakasirika?
Hata kama yule boss ni mdogo kiumri utamnyenyekea
Boss wa wanawake ni Wanaume.
Allah ndivyo alivyoamrisha na kupanga.
Wanawake laiti wangejua cheo hichi, Wallah wa billah akijua bado nusu saa mumewe kurudi,
Wanawake wangeoga, wangejipamba, wakakaa barazani kumsubiri bwana na angekuja kukulaki hata kama umebeba bakora.
Leo yako wapi leo? yako wapi?
Leo mke wako ukimuonesha kidole, mkono wa kushoto anashika mwiko mwingine anashika sufuria na anasema kama mwanaume kweli njoo uone cha mtema kuni.
Usicheke sheikh, Sema "Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un"
Unachekelea nini,Kuna cha kuchekelea.
Hatuna thamani ndugu zangu..
Na nyumba ni mwanamke, Mwanamke akishaharibika huna nyumba wewe.
Wewe huna nyumba na ndio maana leo majumba yameharibika, hujaona?
Mtu ana swali swala 5 lakini watoto wake wanavaa suruali
Kuna suruali mtu akivaa zinakuwa kama amevaa soksi, Hana kauli.
Ukiongea, Watoto atoto wanaenda kwa mama yao umewazuia kuvaa suruali na sisi tunataka kwenda out, sasa sijui itakuaje na huyu Mzee nae na ujahidina wake.
Mama yao anawajibu achaneni nae nitamalizana nae chumbani huyo, Kwani yeye hakupitia kwenye ujana wake..
Yataisha hayo wanangu nendenii,
UMEKWISHA WEWE. Moto unakusubiri, na utaswali wewe na siku ya kiama 0.
Tumeharibikiwa, tuna nini sisi? majumbani kumeoza
Fatma binti wa mtume, siku moja alikaa na mume wake wanazungumza akasema neno moja likamkera mumewe alikasirika..
Fatma alijua thamani ya mume, Fatma ana Dini sio kama wake zetu.
Aliacha kila kitu akaenda mpaka chini ya miguu ya mume wake, akawa analia huku akitamka mume wangu "Nisamehe" × 72
Aliomba radhi Fatma mara 72 hakusamehewa, mara 73 sedinali huruma ikamuingia akamuita eeh Fatma..
..eeh Fatma nimekusamehe ila uchunge ulimi wako, na ujue mimi nani Fatma, Kama wewe hukijui cheo changu! Allah ANAKIJUA.
Fatma akawa analia, sedinali akamuita eeh Fatma nini unalia mbona nimekusamehe! Akajibu sawa wewe umenisamehe, je MUNGU amenisamehee?
Naweza kuangamizwa na Mungu, naomba niruhusu nikamuulize baba mtume Muhammad. Anaenda,
Eeh baba yangu wewe ni nabii wa M/Mungu Leo nilimkera mume wangu wakati tunazungumza, amenisamehe je Mungu amenisamehee?
Mtume akamwambia Fatma "ELEWA RADHI ZA WAUME ZIPO PAMOJA NA MUNGU"
Kama yeye amekusamehe basi Mungu amekusamehe, ila elewa mwanangu laiti ungekufa bila kusamehewa na muwe wako wallah,
Mimi baba yako kwenye jeneza lako nisingesimama, Nisingekuswalia.
Tazameni Thamani ya mume, je wake zetu wanayajua haya? Leo nani anaombwa radhi hapa nani?
Hawezi kusema mume wangu Nisamehe, Bahati hiyo utaitoa wapi?
Zaidi anaweza kukusanya mashoga kuwaambia nimuombe radhi, kwani namuogopa?
Cha ajabu tunavyoishia na wanawake leo, makosa anafanya mwanamke radhi anaomba Mwanaume, unajiita gentleman kuna Mapenzi hapo? Huo ni ushetani
Juzi hapa kulikuwa na sikukuu ya wanawake, siku hizi wanawake wanatoka, wanakwenda kwenye viwanja..Siku hiyo ametaka anaenda hujataka anaenda.
Tena anakwambia kabisa leo niache tafadhari niache, Siku yangu leo, anarudi Saa sita za usiku na mdomoni mwake ananuka harufu ya pombe
anagonga dirisha, bwana mkubwa amelala na watoto sebleni akimsubiri mkewe. Unaita mapenzi hayo? Wewe umelaaniwa na Mungu na kupewa baraka na Shetani.
Unamuuliza ndio unarudi saizi, anakujibu tafadhari Usinisumbue nimechoka napumzika, tutakorofishana, Nitaondoka kwetu Sasa hivi.
Mtu mzima Anapiga magoti kashakuwa dhariri, Nisamehe niko chini ya miguu yako, Nisamehe mke wangu sirudii tena, Jazba tu Ile.. Ikifika Hali hii tuna salama nini?
Bado unaita kujali? kiongozi au wewe ndio unaongozwa, huvijui vifungu vya Quran tunaishia kusoma tu kwenye hitima.
Mwanamke akimjua Mungu, akimjua mtume utapata Utulivu,
Wewe bwana mwenye haraka, wewe bwana usiyetulizana, wewe unaechanganyikiwa na maumbile na picha za mitandaoni, wewe unayetaka kujibu matusi kwa sababu ni dhaifu mbele ya mkeo
Angalia faida ya kuwa na mke mwenye Dini.
Fatma, Mume wake sedinali akiwa anatoka kwenda kutafuta rizki,
Wakati anatoka kwenda kutafuta. Fatma alikuwa akitoka na yeye akisimama mlangoni Kisha anamuhusia mumewe.
Unajua anamwambiaje...
Mume wangu unakwenda kutafuta rizki tafadhari katafute rizki ya halal tu, Usije ukatafuta riziki ya Haram,
Sisi tunaweza kuvumilia hiyo shida na misukosuko ya dunia, hata hiyo njaa Tunaweza kusubiria ila Wallahi Hatuna uvumilivi wala subra ya kuvumilia misukosuko ya akhera .
Ukileta rizki ya Haram tukishakula sisi, Mungu siku ya kiama atatutia Motoni huko hatuwezi kusubiri.
Nenda katafute na Ukikosa Bora urudi Mikono mitupu tutakunywa hata Maji.
Leo ukitoka wewe,
Mkeo anakwambia kabisa si unakumbuka ndio safari yangu eeh, Ukakope, ukanyang'anye, Ukaibe, mpaka urudi na nauli hapa mimi Mwanaume suruali simtaki.
Yaani huyo unayemuita mpenzi wa maisha yako kakupa kibali cha ufanye chochote kafanye tu anachotaka yeye pesa
Fatma angalia maandilizi aliyokuwa anakifanya kumpokea mume wake, alikuwa akichukua ndoo mbili za maji...
Uzi utaendelea kwenye App ya "Ommyfitness" Taarifa zaidi zitakuja
Kama umejifunza kitu follow @ommyfitness
Tembea page zangu Kwa ajili ya Mazoezi
MWISHO.!!

جاري تحميل الاقتراحات...